sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » MASOMO YA NGONO KUANZA KUFUNDISHWA SHULENI

UNGANA NA 
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA

KUNDI la wanaharakati sasa linataka masomo kuhusu ngono yakaguliwe na Wakenya kabla ya kuruhusiwa kufundishwa shuleni.
Kundi hilo linalojulikana kama Sauti ya Wanjiku Jumapili lilisema kuwa masomo hayo yanajumuisha masuala yanayokiuka maadili ya Wakenya.

“Silabasi kuhusu masuala ya ngono iliandaliwa na mashirika ya kigeni bila kuzingatia maadili yatu ya kiafrika. Baadhi ya masuala yaliyomo kwenye silabasi hiyo ni namna watoto wa kuanzia umri wa miaka sita wanaweza kutangamana na wenzao ambao walibadilisha jinsia au wanajihusisha na ushoga,” akadai mshirikishi wa kundi hilo Dkt Francis Kuria.

Kwa mujibu wa wanaharakati hao waliokuwa wakihutubia wanahabari jijini Nairobi, serikali ilikubali kufundisha wanafunzi silabasi hiyo kwa lengo la kutaka ufadhili kutoka kwa mataifa ya kigeni.

“Wakenya hawakuhusishwa katika maandalizi ya masomo hayo ambayo huenda yakahatarisha maadili ya watoto shuleni. Hatuwezi kuruhusu mataifa ya Magharibi kutuamulia masuala yanayopaswa kufundishwa shuleni ,” akasema Dkt Kuria.

Kulingana na wizara ya Elimu, masomo kuhusu ngono inalengakukabiliana na visa vya watoto kupata mimba za mapema na kujizuia kutokana na maradhi ya Ukimwi.

Wanaharakati hao pia walishutumu wizara ya Elimu na Taasisi ya Uendelezaji wa Mtalala nchini (KICD) kwa kutohusisha wananchi katika maandalizi ya mfumo mpya wa elimu wa 2-6-3-3-3 unaotarajiwa kuchukua mahali pa 8-4-4.

“Mswada wa mfumo mpya unafaa kuwekwa wazi ili uweze kukaguliwa na Wakenya badala ya kuhusisha washikadau wachache pekee katika mahoteli ya kifahari. Katiba inahitaji kuwa wananchi wanahusishwa kikamilifu katika maamuzi muhimu hivyo, Wakenya ni lazima washirikishwe katika mfumo mpya wa elimu,” akasema Dkt Kuria.

Kongamano la wataalamu
Mnamo Machi, zaidi ya wajumbe 500 wakiwemo wataalamu wa kimataifa walikongamana jijini Nairobi kujadili mtalaa mpya ambao umekuwa ukiandaliwa na taasisi ya KICD kwa muda wa mwaka mmoja sasa.

“Hatupingi kuanzishwa kwa mfumo mpya wa Elimu lakini tumegundua baadhi ya watu walipenyeza baadhi ya masuala yasiyofaa katika silabasi hivyo tunataka Wakenya wote kutoa maoni yao kabla ya kuanza kutekelezwa,” akasema mwanachama wa Sauti ya Wanjiku Bi Anne Musomba.


Kulingana na Waziri wa Elimu Fred Matiang’i, mfumo mpya wa elimu unatarajiwa kuidhinishwa na kongamano la kitaifa Julai.

Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call

Karibuni sana
LINK CLASSIC

LIKE PAGE ZETU 



"KWA HABARI ZAIDI "

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply