UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Republican Donald Trump amefikisha idadi ya wajumbe ya kupata uteuzi wa chama hicho kulingana na chombo cha habari cha AFP.
Bw Trump ambaye aliwashinda wagombea wengine 16 wa chama hicho ameripotiwa kupata wajumbe 1,238 mmoja zaidi ya inavyohotajika.
Chama cha Republican kinataraijiwa kukamilisha uteuzi wao katika mkutano wa chama hicho utakaofanyika huko Cleveland mnamo mwezi Julai.
Iwapo atathibitishwa ,bw Trump atakabiliana na aliyekuwa waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Hillary Clinton au seneta wa Vermont Bernie Sanders ambao wanashindania uteuzi wa chama cha Demokrat.
Siku ya Jumatano,bilionea huyo wa New York alipanga kufanya mjadala na Bernie Sanders katika runinga mjini California kabla ya uchaguzi wa mchujo wa tarehe 7 mwezi Juni.
Bw Sanders alikubali kushiriki katika mjadala huo katika ujumbe wake wa Twitter uliosema: ''Game on''.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii
Mungu akubariki, bila kusahau kuwashirikisha rafiki zako kutembelea website
hii.
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow
hapa chini
+255 (0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK
CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
"FOR
MORE INFO PLEASE"
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: