UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
Watu saba kati ya 13 waliokuwa wameshtakiwa kuhusiana na mashambulio ya mabomu ya mwaka 2010 mjini Kampala wamepatikana na hatia.
Mashambulio hayo, yaliyotekelezwa katika maeneo mawili watu walipokuwa wakitazama fainali ya Kombe la Dunia, yalisababisha vifo vya watu 74.
Jaji Alfonse Owiny-Dollo ameamua watu sita kati ya walioshtakiwa hawakuwa na hatia.
Jaji, akitegemea sana ushahidi wa watu wawili waliokiri kuhusika na kuhukumiwa, alisema Isa Ahmed Luyima ndiye aliyehusika sana katika mashambulio hayo.
Kundi la al-Shabab kutoka Somalia lilidai kuhusika.
Jaji awali aliwaondolewa mashtaka ya kuwa wanachama wa kundi la kigaidi akisema kundi la al-Shabab wakati huo halikuwa limeorodheshwa kuwa kundi la kigaidi nchini Uganda.
Waliopatikana na hatia ni: Isa Ahmed Luyima, Hassan Haruna Luyim, Habib Suleiman Njoroge, Suleiman Hajjir Nyamandondo, Idris Magondu, Hassan Hussein Agade na Muhammed Ali Muhammed.
Walioondolewa mashtaka ni Omar Awadh Omar, Muzafar Luyima, Abubakari Batemyeto, Yahya Suleiman Mbuthia, Muhammed Hamid Suleiman na Dkt Kalule Suleiman.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii
Mungu akubariki, bila kusahau kuwashirikisha rafiki zako kutembelea website
hii.
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow
hapa chini
+255 (0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK
CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
"FOR
MORE INFO PLEASE"
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: