UNGANA NA
LINK CLASSIC
KATIKA KIPENGELE CHA
HOT NEWZ
SERIKALI ya Awamu ya Tano imeanza kutekeleza kwa vitendo azma yake ya kujenga uchumi unaotegemea viwanda baada ya kuzindua ujenzi wa mradi maalumu wa uwekezaji wa viwanda mkoani Morogoro ili kukuza uchumi na kuongeza ajira nyingi kwa vijana nchini.
Utekelezaji huo ni kutokana na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage juzi kuzindua eneo maalumu la ujenzi wa miradi ya uwekezaji la Star City katika Manispaa ya Morogoro.
Eneo hilo la miradi ya uwekezaji lina ukubwa wa ekari 10,661 na lilikuwa ni shamba la mkonge Tungi Sisal Estate ambalo kwa sasa likijulikana kwa jina la Dominio Plantation Limited (DPL).
Waziri Mwijage kabla ya kuzindua eneo hilo maalumu la uwekezaji, alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli imeanza utekelezaji wa Tanzania kuwa nchi ya viwanda kwa kuanza na Mkoa wa Morogoro.
“Morogoro haijapendelewa isipokuwa ina historia tangu wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambapo Waziri Jamal (Amir) aliwezesha kujengwa kwa viwanda hivi hapa Morogoro,” alieleza Mwijage na kuongeza: “Morogoro ina bahati ya kuwa na sifa ya kujenga viwanda kutokana na mazingira na jiografia yake naweza kusema ina bahati ya kuzaliwa ilivyoumbwa na Mungu kuvutia uwekezaji.”
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz
ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua
LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau
kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia
waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
Whatsapp
+255 652 989 873
Karibu
sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: