UNGANA NA
LINK CLASSIC
KATIKA KIPENGELE CHA
HOT NEWZ
Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wanaonekana kurejesha matumaini yao kuhusu kumalizika kwa adha ya usafiri jijini humo, hii ni kutokana na kukamilika kwa mradi wa mabasi yaendayo haraka ambapo jana zilitangazwa nauli za mabasi hayo, na hii leo mabasi hayo yameanza majaribio kwa kubeba abiria kwa muda wa siku mbili bure wakati akisubiriwa Rais Magufuli kuuzindua mradi huo rasmi Alhamisi wiki hii.
JINSI YA KUKATA TIKETI ZA MABASI HAYO
Kutakuwa na mifumo miwili ya ukataji tiketi, mfumo wa kwanza ni ule uliozoeleka wa tiketi za karatasi ambazo unakata ukiwa katika kituo cha mabasi hayo, na wapili ni ule wa kutumia KADI MAALUMU, Huu ni mfumo ambao abiria atapatiwa kadi na kujaza salio kwenye kadi hiyo kupitia mawakala watakaotangazwa kwa kuweka kiwango cha nauli ambayo ataweza kuitumia ndani ya wiki au mwezi mzima.
Baada ya hapo abiria atakapofika kituoni atalizimika kuipitisha juu ya mashine maalumu zilizopo kituoni hapo, kwa ajili ya makato ya nauli na ndipo mlango utajifungua kumruhusu abiria kuingia kwenye sehemu ya kusubiria usafiri huo.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa
kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia
endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya
Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea
website hii
Pia
waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
+255
(0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA


No comments: