UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Tanzania ina mpango wa kujenga njia ya umeme kutoka Mbeya hadi Zambia kupitia Tunduma ili kupunguza tatizo la umeme linaloikabili nchi hiyo.
“Serikali ya Tanzania inajenga njia ya umeme ya msongo wa KV
400 kutoka Iringa – Dodoma – Singida – Shinyanga ambayo ni sehemu ya mradi mkubwa wa umeme unaolenga kuunganisha Zambia, Tanzania na Kenya,” alisema.
Alisema upembuzi yakinifu kwa ajili ya KV400 kutoka Iringa hadi Mbeya, umekamilika tangu mwaka 2012, na hivi sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuunganisha kipande cha kutoka Mbeya na gridi ya Taifa ya Zambia.
Waziri Mkuu ambaye anahudhuria katika Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwenye Kituo cha Mikutano cha Mulungushi kilichopo Lusaka, Zambia kwa niaba ya Rais John Magufuli, alitoa ufafanuzi huo jana mchana wakati akichangia hoja kwenye mjadala wa wakuu wa nchi na Serikali uliohusu Nishati na Mabadiliko ya Tabianchi kwenye ukumbi wa mikutano cha kimataifa wa Mulungushi.
Alisema ili kukabiliana na changamoto ya nishati barani Afrika, nchi za bara hili zinahitaji kuwa na fedha ama mitaji, teknolojia ya kisasa na wataalamu wenye ujuzi wa kutosha, jambo ambalo amesema ni gumu kulikamilisha kila nchi peke yake.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii
Mungu akubariki, bila kusahau kuwashirikisha rafiki zako kutembelea website
hii.
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow
hapa chini
+255 (0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK
CLASSIC
"FOR MORE
INFO PLEASE"
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: