sponsor

Slider

EMBROIDERY, DTF, & SCREEN PRINTING - T-shirt, Overall, Shirt , Pylon, Kofia Nk..


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » POLEPOLE : NIMEMFAHAMU RAIS MAGUFULI KABLA HAJAWA RAIS

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema kuwa amemfahamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kabla hajawa Rais wa Tanzania.
Akizungumza na Azam News, Polepole amesema kuwa Rais huyo ni msikivu anasikiliza ushauri kwenye vikao anaacha wajumbe waseme kisha yeye anasikiliza hoja ambayo wajumbe wanataka.

“Mimi nimemfahamu Rais Magufuli kabla hajawa Rais wa Tanzania, nimemfahamu akiwa Waziri nimemfahamu akiwa anatafuta kugombea CCM akapewa dhamana kwenye kampeni amekuwa kiongozi wangu kwenye serikali na sasa ni kiongozi wangu kwenye chama na sasa ni kiongozi wetu wa nchi kama ni mtu mmoja namfahamu ni msikivu anasikiliza ushauri mnapokaa kwenye vikao mnaacha wajumbe waseme kisha yeye atasikiliza hoja kwa kwenda ile ambayo wajumbe wanataka ni Magufuli sasa mtu unapokwenda kutoa kauli ya kumaliza mjadala kwamba huyu hasikilizi ushauri tenda haki uwe mwanifu hata kufa Mungu wetu wa mbinguni atakupa taji ya uzima,” alisema Polepole.
Aidha Polepole alizungumzia baadhi ya viongozi wa dini kuzungumzia siasa ambapo alisema “Viongozi wetu wa dini wanahudumumia Mungu na watu wake kauli kamilishi isiyokuwa na ushahidi ni kitu kibaya ukisema huyu mbona amekamatwa kwa mambo mabaya amekamatwa kwasababu ni mhalifu anatuhumiwa kwa uhalifu katoa lugha ya kichochezi, Tanzania, Marekani mpaka China ukitoa lugha ya uchochezi ni kosa la jinai na anaekushtaki siop Rais ni kwa mujibu wa sheria na ni jamhuri inayokushtaki wewe.”

jiunge na group la whatsapp  kupata habari haraka bofya hapa
KWA HABARI ZAIDI

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply