UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
Kutokana na madudu yaliyofanywa na NIDA hapo awali kunaifanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuridhia kuiazima Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mitambo yake kwa muda wa siku 90 ili iweze kuchakata upya taarifa katika zoezi linalotazamiwa kuanza hivi karibuni la utoaji wa vitambulisho vipya vya taifa.
Ambapo mapema leo Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa nchini (NIDA) imesema kuwa ifikapo Desemba 31 mwaka huu itatoa Namba ya utambulisho itayowezesha kila mwananchi kuweza kutambulika ilikuweza kurahisisha huduma mbalimbali ikiwemo shughuli za usafiri wa ndani na nje ya nchi .
Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji Vitambulisho Alphonce Malibiche amesema kuwa mamlaka hiyo inatarajia kusambaza mawakala wake wapatao 106 katika maeneo mbalimbali ikiwemo vijijini ili kuweza kurahisisha zoezi la upatikanaji wa vitambulisho vya taifa .
‘’Tunatarajia kusambaza mashine 5600 kwajili ya uandikishaji wa vitambulisho katika maeneo mbalimbali vijijini ambapo jumla ya maafisa 106 watahusika katika utekelezaji wazoezi hili hivi karibuni ambapo mfumo huu wa uandikishaji utajumuisha mifumo ya uandikishaji wa tume ya uchaguzi ‘’.Alisema Malibiche .
Malibiche ameongeza kuwa kufuatia kusimamishwa kwa vijana waliokuwa wanasimamia zoezi la uandikishwaji wa vitambulisho vya Taifa katika mamlaka hivyo watawaipa stahiki zao kuanzia jumatano ya wiki ijayo, huku akiongeza kuwa taasisi yake haina ubaguzi katika utoaji wavitambulisho ambapo ucheleweshwaji wa baadhi ya vitambulisho kwa wananchi unatokana na kuhakiki taarifa zilizo jazwa awali ikiwemo umri pamoja na makazi ya muhusika .
Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call
Karibuni sana
LINK CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
"KWA
HABARI ZAIDI "
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: