UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
Mwaka 2001 Zanzibar iliingia katika machafuko yaliyopelekea watu kuuawa kutokana na vurugu za kisiasa, hivyo kutokana na historia hiyo Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) kimetaka wananchi wa Zanzibar kudumisha umoja wao na kuachana na kufuata kauli za baadhi ya viongozi wa kisiasa wanaochochea vurugu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa TLP, Agustino Lyatonga Mrema amesema kauli za viongozi wa siasa visiwani humo zinachochea kuvuruga amani, na kuwataka wananchi kuzipuuza kwani hakuna aliye juu ya sheria hivyo kuwepo kwa watu wanaochochea kuvuruga waangaliwe kama wahaini na hatua zichukuliwe dhidi yao katika kuhakikisha wananchi wanakuwa salama.
“Hata nchi wahisani waache kuingilia mambo yetu ya ndani kwani wao hawaishi huku na hata mauaji yakitokea hawaguswi kwa lolote”.Alisema Mrema
Mrema amesisitiza suala la uchochezi liangaliwe kwa macho mawili dhidi ya watu wanaotaka kuvuruga amani katika mazingira hayo, kwani Mahakama ya ICC haiangalii viongozi wa serikali na hata viongozi wa kisiasa ambao kwa namna moja wanakuwa wamehusika katika kusababisha mauaji kutokana na kauli wanazozitoa.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii
Mungu akubariki, bila kusahau kuwashirikisha rafiki zako kutembelea website
hii.
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow
hapa chini
+255 (0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK
CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
"FOR
MORE INFO PLEASE"
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: