sponsor

Slider

EMBROIDERY, DTF, & SCREEN PRINTING - T-shirt, Overall, Shirt , Pylon, Kofia Nk..


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » MAHAKAMA YATUPA PINGAMIZI DHIDI YA KAFULILA

UNGANA NA
LINK CLASSIC
KATIKA KIPENGELE CHA
HOT NEWZ

FERINAND Wambari, Jaji wa Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora  ametupilia mbali hoja za mawakili wa Husna Mwilima, Mbunge wa Kigoma Kusini na serikali dhidi ya David Kafulila ambapo waliwasilisha nyaraka za kurasa zaidi ya 300 kuomba kesi aliyoifungua Kafulila mahakamani hapo ifutwe.

Katika hoja zilizowasilishwa na mawakili wa Mbunge Mwilima wamesema, baada ya Kafulila kuwasilisha vielelezo na mashahidi watatu mahakamani hapo hawaoni kesi ya kujibu .

Akifuta hoja hizo mahakamani Jaji Wambari amesema, Husna anapaswa kutoa ushahidi uliompa ushindi na kuagiza msimamizi wa uchaguzi huo kutoa ushahidi uliopelekea kumtangaze Husna Mwilima kama mshindi wajimbo hilo.

Baada ya kauli hiyo, Jaji Wambari ameahirisha kesi hiyo na kuagiza kusikilizwa tena Mei 3 mwaka huu.

Awali, Kafulila alikuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini ambapo mahakama iliamuru chini ya Jaji Wambari kuwasilishwa fomu halisi za Matokeo ya Uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Kafulila alikubali na akaiomba mahakama kuiamrisha NEC kuwasilisha fomu hizo mahakamani ili ziweze kupitiwa kwa kulinganishwa na fomu alizowasilisha mahakamani na kupelekea Kenned Fungamtama, Wakili wa Serikali kupinga ombi hilo hapo awali.

Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka jana, Kafulila alidai  ndiye mshindi halali wa kiti cha ubunge jimboni hapo lakini Msimamizi wa Uchaguzi alimtangaza Husna kuwa mshindi kutoka CCM badala yake.


LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini

Whatsapp +255 652 989 873



PINTEREST  TWITTER    

LINKEDIN     DRIBBBLE

Karibu sana


LINK CLASSIC

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply