UNGANA
NA
LINK
CLASSIC
KATIKA
KIPENGELE CHA
HOT NEWZ
WAZIRI wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mwigulu Lameck Nchemba amesema baadhi ya maofisa ushirika wamekuwa ni tatizo kwa kutumia vibaya mamlaka yao kushiriki kuhujumu na kudhoofisha Vyama vya Ushirika.
Waziri Mwigulu alisema hayo Mjini Moshi katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Gelazius Kamanzi kwenye ufunguzi wa Mafunzo ya Maofisa Ushirika kutoka Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.
“Ofisa Ushirika kuchukua mkopo wa fedha au pembejeo kutoka kwenye chama cha ushirika wakati sio mwanachama ni mfano mbaya kwa viongozi na wanachama wa ushirika,” alisema na kuongeza: “Vile vile, zipo tuhuma kwamba baadhi yenu mnaomba rushwa ili muweze kutekeleza wajibu wenu.Tatizo hilo la rushwa lipo pia kwa viongozi na watendaji wa vyama vya ushirika na wakati mwingine hufanyika kwa kushirikiana na baadhi yenu.”
Mafunzo hayo yameandaliwa na Tume ya Maendeleo ya Ushirika kwa maofisa ushirika, yatafanyika kikanda nchi nzima kwa lengo la kuwajengea uwezo wa usimamizi na udhibiti wa vyama vya ushirika, uhamasishaji wa maendeleo ya ushirika na uandaaji na uwasilishaji wa takwimu za vyama vya ushirika na umuhimu wake.
Matatizo mengine yaliyoelezwa na Waziri Mwigulu na kuagiza yakomeshwe ni pamoja na vyama kutowalipa wanachama wao fedha zao zote za mauzo ya mazao, wanachama kuongezewa madeni wasiyokopa kama ya pembejeo.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz
ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua
LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau
kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia
waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
Whatsapp
+255 652 989 873
Karibu
sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: