
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Mwanza kimeunda kamati kuchunguza tuhuma dhidi ya baadhi ya walimu wa Shule ya Sekondari Mihama wilayani Ilemala kujamiiana na wanafunzi wao.
Mwenyekiti wa CWT mkoani hapa, Sibora Kisheri alisema wameunda kamati hiyo baada walimu wanane, akiwamo mkuu, Joseph Marifedha kusimamishwa kazi kwa amri ya aliyekuwa Mkuu wa mkoa huo, Magessa Mulongo kwa tuhuma hizo.
“Haiingii akilini kuona walimu wote wakawa na sifa ya makosa yanayofanana, hivi hakuwapo hata mmoja aliyeshtukia mchezo huo na kuwashauri wezake,” alisema Kisheri.
Alisema uchunguzi huo unalenga kubaini kiini cha tuhuma hizo na kuishauri Serikali na vyombo husika hatua stahiki za kuchukua kuhakikisha kila upande unatendewa haki.
Aliwaasa walimu kufuata sheria, kanuni na misingi ya kazi kwa kutimiza wajibu na kuepuka mambo yanayokinzana na taaluma hiyo.
Hivi karibuni Mulongo aliwasimamisha walimu hao baada ya kupata taarifa kuwa walikuwa wakijihusisha na vitendo hivyo.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa
kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia
endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya
Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea
website hii
Pia
waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
Karibu sana
LINK
CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA


No comments: