sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » TETESI ZA SOKA ULAYA



Kiungo wa kati wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, ataitaka klabu hiyo kukataa ombi lolote kutoka kwa PSG huku mchezaji huyo wa Brazil akitafuta kujiunga na Barcelona. (Sport via Daily Mail)

Mkufunzi wa Tottenham Mauricio Pochettino anamchunguza mchezaji wa Argentina na West Ham mwenye umri wa miaka 24 Manuel Lanzini. (Mirror)



Beki wa kulia wa Arsenal Bellerin, 22, anasakwa na Juventus na tayari imebainika kwamba klabu hiyo imewasiliana na beki huyo wa Uhispania kupitia wawakilishi wake.. (Sun)

Paris St-Germain wanamtaka beki wa Barcelona's mwenye umri wa 33 Javier Mascherano. (Diario Gol via Talksport)



Mshambuliaji wa Chelsea, raia wa Uhispania Alvaro Morata, 25, amesema kuwa yuko tayari kurudi Real Madrid licha ya kuuzwa na mabingwa hao wa Ulaya chini ya miezi minne iliopita. (Mirror)

Manchester United watawaongezea kandarasi wachezaji wake Juan Mata, Ander Herrera, Ashley Young na Daley Blind hadi mwisho wa msimu ujao.(Telegraph)



Mshambuliaji wa Manchester City Gabriel Jesus, 20, anaamini kwamba ana kazi ya ziada kupata fursa ya kushirikishwa katika kikosi cha Brazil cha kombe la dunia licha ya kulifungia taifa lake bao la lala salama katika mechi ya kirafiki dhidi ya Japan. (Goal)

Everton italazimika kuongeza maradufu mshahara wa mkufunzi wa Burnley Sean Dyche, 46, ili kujaribu kumchukua kujaza pengo lililowachwa wazi katika uwanja wa Goodison Park. (Daily Mirror)



Kiungo wa kati wa Bayern Thiago Alcantara, 26, amesema kuwa yuko tayari kurudi katika klabu ya Barcelona, klabu ambayo mchezaji huyo wa Uhispania aliondoka 2013 lakini amesisitiza kuwa anafurahia kusalia Ujerumani.. (sun)

Stoke City inataka kuwasajili kwa mkopo wachezaji Harry Souttar, Ollie Shenton na Danny Jarvis. (Stoke Sentinel)



Manchester United wamejiandaa kusikiza maombi ya zaidi ya £20m kumuuza beki Luke Shaw ,22, mnamo mwezi January. Klabu hiyo ya Jose Mourinho itajaribu kumuuza mwaka mmoja mapema ili kumzuia kuondoka kwa kitita cha chini. (Daily Mail)

Arsenal imewatuma wasajili wake kumchunguza kinda wa Manchester United Bobby Duncan akicheezea timu ya Uingereza ya wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 wiki hii.Duncan ni binamu yake mchezaji wa zamani wa Liverpool Steven Gerrard. (Daily Mirror)

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply