Rais wa Marekani Donald Trump amekishutumu kituo cha habari cha CNN kwa kusambaza habari za uongo kuhusu Marekani ulimwenguni.
Rais Trump katika mtandao wake wa twitter ameandika kuwa CNN ni "Fake News ".
Kwa mujibu wa habari,Trump ametoa sifa kwa kituo cha habari cha Fox News na kusema kuwa ni kituo kinachoheshimika zaidi Marekani.
Trump ameongeza kwa kusema japokuwa CNN haina heshima kubwa Marekani ,inatizamwa na ulimwengu mzima na hivyo kupotosha nchi nyingine kuhusu Marekani.
Hata hivyo kitengo cha mawasiliano cha CNN kimeijibu twitter ya Trump na kuandika,"Sio kazi yetu kuiwakilisha Marekani ulimwenguni,ni kazi yako wewe.Sisi tunafikisha habari tu".
Trump amekuwa akikishambulia kituo hicho cha habari kwa muda sasa.
KWA HABARI ZAIDI
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: