sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » SERIKALI KUNUNUA NDEGE TATU

UNGANA NA 
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA

SERIKALI imetangaza kutenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa meli mpya katika maziwa nchini, ununuzi wa ndege tatu mpya, ujenzi wa reli ya kisasa na kulipa deni la Bohari ya Madawa (MSD).

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango akiwasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/17 bungeni jana, alisema serikali itaendelea kukabiliana na kero zinazotokana na uchakavu wa miundombinu ya reli, barabara, bandari na viwanja vya ndege.

“Katika mwaka 2016/17, serikali imetenga shilingi trilioni 5.47 sawa na asilimia 25.4 ya bajeti yote ukiondoa Deni la Taifa, kwa ajili ya miradi ya ujenzi na uchukuzi,” alieleza Dk Mpango.

Aliyataja baadhi ya maeneo yanayohusika ni ujenzi wa miundombinu ya barabara – kiasi cha Sh trilioni 2.18 kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hasa zenye kufungua fursa za kiuchumi na kukarabati barabara zilizopo, kiasi cha Sh trilioni 2.49 kimetengwa kwa ajili ya kuanza kujenga Reli ya Kati kwa kiwango cha standard gauge, ununuzi wa ndege mpya tatu za abiria na ununuzi wa meli mpya Ziwa Victoria.

Nyingine ni ukarabati wa meli katika Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika; uboreshaji wa miundombinu ya bandari; na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege. Aidha, kiasi cha Sh bilioni 161.4 kimetengwa katika Mfuko wa Reli kwa ajili ya ununuzi wa mabehewa na vichwa vya treni pamoja na ukarabati wa reli.

Aidha, alisema serikali imetenga jumla ya Sh trilioni 1.13 sawa na asilimia 5.3 ya bajeti yote bila kujumuisha Deni la Taifa ili kugharimia upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa ajili ya matumizi ya majumbani na viwandani.

Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call

Karibuni sana
LINK CLASSIC

LIKE PAGE ZETU 



"KWA HABARI ZAIDI "

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply