sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » MUFTI MKUU-WAISLAMU TUOMBEE AMANI YA NCHI

UNGANA NA 
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA

WAKATI Waislamu duniani kote wakitarajia kuanza kutekeleza moja ya nguzo tano za dini yao kwa kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani, Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limewataka Waislamu nchini kutumia mwezi huo, kuombea amani na utulivu.

Aidha, wametakiwa kuhimizana kufanya kazi hasa katika kipindi hiki ili kupata riziki za halali kama kaulimbiu ya Rais John Magufuli ya ‘Hapa Kazi Tu’ inavyosema kwa kaulimbiu hiyo si tu ni ya Rais, bali ni agizo la Mwenyezi Mungu kupitia kitabu chake Kitakatifu cha Kurani.

Hayo yameelezwa na Mufti na Shehe Mkuu wa Tanzania, Abubakar bin Zubeir wakati akizungumza kwenye Kongamano la kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, lililofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Mufti Zubeir alisema Rais Magufuli anaposema ‘Hapa Kazi Tu’ anakuwa amezungumzia dini moja kwa moja kwani hata katika Kitabu Kitukufu cha Kuran, Mwenyezi Mungu amesema anapendezwa na watu wanaofanya kazi.

“Kwa hiyo watu wahimizane kufanya kazi sana hasa katika kipindi hiki ili kupata riziki halali itakayowawezesha kupata mahitaji yao ya futari na daku,” alisema Mufti Zubeir. Aidha, aliwataka Waislamu kusaidiana ili kila mmoja afurahie mwezi wa Ramadhani.

Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call

Karibuni sana
LINK CLASSIC

LIKE PAGE ZETU 



"KWA HABARI ZAIDI "

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply