UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA
Jaji Mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed Othman Chande amesema tafiti ambazo zimefanywa na taasisi mbili nchini zimeonesha kuwa idara ya mahakama bado inakabiliwa changomoto kubwa ya ukosefu wa nidhamu, huku tatizo la rushwa pia likitajwa kuwa kero
Mhe. Jaji Mkuu ameyasema hayo mjini Musoma mkoani Mara, wakati akizungumza na watumishi wa idara ya mahakama za mkoa wa mara, ambapo amesema tafiti hizo ambazo zimefanywa na idara ya mahakama yenyewe kupitia taasisi hizo, zimebaini rushwa na vitendo vya utendaji mbovu kwa baadhi ya watumishi wa idara ya mahakama vimelalamikiwa kwa kiasi kikubwa na wananchi.
Hata hivyo Jaji mkuu amemweleza mkuu wa mkoa wa Mara, kuhusu mipango ya ujenzi wa mahakama kuu mkoani mara, hatua ambayo amesema mbali na kuwapunguzi kero wananchi pia itarahisha upatikanaji wa haki kwa wakati.
Katika ziara hiyo Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Mohamed Othman Chande, pamoja na kukutana na viongozi mbalimbali wa serikali na idara ya mahakama, pia amepata fursa ya kutembelea mahakama za mwanzo, wilaya na mkoa pia eneo linalotarajia kujengwa mahakama kuu mkoani mara.
Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call
Karibuni sana
LINK CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
"FOR
MORE INFO PLEASE"
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: