sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » KWANINI WAKULIMA WANAKOSA MIKOPO ?

UNGANA NA 
LINK CLASSIC
KATIKA KIPENGELE CHA 
HOT NEWZ

Asilimia 80 ya uchumi wa Tanzania unategemea sekta ya kilimo kama chanzo kikubwa cha mapato yake, pamoja na hayo  serikali  imeendeleza jitihada zake za kuwakwamua wakulima kwa kutenga fungu la kutosha ili kuhakikisha sekta hiyo inazidi kukua na kuendelea kuwa msaada mkubwa kwa Watanzania.

Pamoja na jitihada hizo kumekuwepo na changamoto kadha wa kadha kwa wakulima hali inayoifanya Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini kuingilia kati ili kupatia ufumbuzi changamoto zilizopo huku ikiwataka wakulima kuunda vikundi ili waweze kupatiwa mikopo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema  leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo, Thomas Samkyi amesema ukosefu wa taarifa za mauzo ya mazao kwa baadhi ya wakulima ili kuweza kupatiwa mikopo imekuwa ni kikwazo kikubwa kinachowakwamisha wakulima wengi.

“Wakulima wengi hawana taarifa sahihi za mapato zinazotokana na mazao hali inayosababisha taasisi nyingi za kifedha kushindwa kuwapatia mikopo kwa wakulima” Alisema Samkyi .

Samkyi amesema kutojihusisha kwa wakulima katika vikundi ili kupatiwa mikopo imekuwa kikwazo kikubwa kwa wakulima hao kuweza kupatiwa mikopo yenye masharti nafuu kutokana na kuweka dhamana ya nyumba zisizo na ubora ili  kupatiwa mikopo hiyo hali inayochangia  kunyimwa mikopo katika taasisi za fedha.

“Wakulima wengi wamekuwa na nyumba ambazo hazina ubora wala hati hali inayochangia wakulima wengi kutoweza kupatiwa mikopo”  aliongeza Samkyi.

LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini

+255 (0) 652989873 whatsapp

TWITTER    
LINKEDIN     DRIBBBLE

Karibu sana
LINK CLASSIC

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply