UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KUPATA HABARI ZAIDI
Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kimeeleza kufadhaishwa na habari zilizochapishwa na magazeti ya Dira ya Mtanzania Toleo la 419 pamoja na Sema Usikike Toleo la 003047 ya Mei 23 mwaka huu kuhusu tuhuma dhidi ya ubadhirifu wa kutisha kwenye chuo hicho.
Emmanuel Mjema Mkuu wa chuo hicho ametoa rai hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Vyombo vya Habari nakusema tuhuma kuhusu ubadhirifu wa kutisha wa milioni 400 si za kweli na zinalenga kuchafua taswira ya chuo hicho ambapo wanachuo hawalipi fedha taslimu na hakuna wanaopewa vyeti wakiwa wanadaiwa ada kama ilivyoelezwa na magazeti hayo.
Aidha amesema tuhuma zinasema walificha ukweli na kuna dalili walipokea rushwa ili wasitoe ripoti kuhusu ubadhilifu walioubaini wa zaidi ya milioni 400 na malipo ya thamani ya shilingi 924,920,668.86 kulipwa bila kuidhinishwa na mamlaka husika.
“Chuo kinafanyiwa ukaguzi wa hesabu zake na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) na kwa kipindi cha miaka minne tumepata hati safi (clean audit report) kuanzia mwaka 2010/2011 hadi 2014/2015.”Amesema Mjema.
Pia amesema chuo hicho kilifanyiwa ukaguzi na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi Serikalini (PPRA) mwaka unaoishia 2014/2015 na chuo kupata alama 95.8 hivyo kuwa moja kati ya taasisi za umma zinazofanya vizuri katika kuzingatia sheria na kanuni za manunuzi ya umma.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii
Mungu akubariki, bila kusahau kuwashirikisha rafiki zako kutembelea website
hii.
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow
hapa chini
+255 (0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK CLASSIC
LIKE PAGE ZETU
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: