WAKATI zaidi ya watu 150 wakijitokeza kuhakiki silaha zao, kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi, Diwani Athumani amesema uhakiki huo sasa unafanyika nchi nzima.
Kamishna Athumani amesema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, huku akikataa kutaja majina ya vigogo waliojitokeza kuhakiki silaha zao kwa sababu za kiusalama.
“Baada ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kufanya uhakiki wa silaha zake hivi karibuni, watu zaidi ya 150 wakiwemo viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wastaafu, mabalozi na wabunge wa nchi mbalimbali wamejitokeza,” alisema.
Mbali na vigogo hao, Kamishna Athumani amesema wananchi wengine wameonesha nia ya kufanya hivyo na kusisitiza kuwa, lengo la uhakiki wa silaha hizo ni kuboresha hali ya usalama kwa kuwajua watumiaji .
Alifafanua kuwa utambuzi huo unafanyika kwa kuwa kunaweza kutokea sababu mbalimbali zitakazofanya wamiliki wa awali wasiendelee kumiliki silaha hizo, ikiwemo vifo na ulemavu.
LINK
CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz ni moja
ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua LEBAL
zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau
kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
Karibu sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA



No comments: