MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela amewataka wakazi wa kata ya Mwakata, wilayani Kahama ambao waliahidiwa kujengewa nyumba na serikali baada ya kuathiriwa na mvua ya mawe kuvuta subira wakati serikali iliyopo madarakani ikitekeleza ahadi iliyotolewa.
Serikali ya awamu ya nne iliahidi kujenga nyumba 342 za walioathirika na mvua ya mawe iliyosababisha zaidi ya watu 48 kupoteza maisha.
Akizungumza na wakazi wa Kata ya Mwakata siku tatu baada ya kuripoti katika kituo kipya cha kazi, Kilango alisema kuwa ucheleweshwaji wa ujenzi ulitokana na Serikali kuelekeza nguvu kufanikisha uchaguzi mkuu uliopita.
Mkuu huyo Mpya wa Mkoa wa Shinyanga alisema kuwa kutokana na uchaguzi huo kuisha kwa sasa Serikali itahakikisha kuwa hakuna mkazi yeyote wa kata ya Mwakata atakayeendelea kuishi kwa jirani.
“Kwa sasa uchaguzi umepita na tuiachie Serikali ifanye kazi yake ya ujenzi wa nyumba hizo na mimi ninawaahidi kuwa nitasimamia ujenzi huo, kwani maafa kama haya yalishawahi kutokea katika jimbo langu za Same enzi za ubunge wangu na Serikali ilichukua muda wa miaka miwili kutatua tatizo kama hilo”, alisema Kilango.
LINK
CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz ni moja
ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua LEBAL
zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau
kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
Karibu sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA



No comments: