sponsor

Slider

EMBROIDERY, DTF, & SCREEN PRINTING - T-shirt, Overall, Shirt , Pylon, Kofia Nk..


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » MAGARI 1,400 YATEKETEA KWA MOTO

Na mashirika ya kimataifa
MOTO mkubwa umeharibu takriban magari 1,400 kwenye jengo la ghorofa la kuegesha magari huko Liverpool nchini Uingereza  na baadhi ya watu kulazimika kuukaribisha mwaka mpya  kwenye makao ya mengine ya muda.
Baadhi ya magari  kati ya 1400 yaliyoteketea kwa moto mapema hii leo.
Wazima moto wanasema  moto huo  uliotokea katika jengo la King's Dock karibu na ukumbi wa Liverpool Echo Arena, ni moto mbaya zaidi kuwahi kukabiliana nao
Polisi wamesema uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa moto kutoka kwa gari moja ulisambaa kwenda kwa mengine.
Watu walihamishwa kutoka  katika majengo yaliyo karibu na jengo hilo  kutokana na moshi.
Polisi wa Merseyside wamesema  magari ya kuzima moto 21 yalikuwa eneo hilo na huku  wazima moto wakisema  kuwa wanachukua  tahadhari ya jengo hilo kuporomoka.
Kwa mujibu wa polisi magari yote yaliyokuwa kwenye jengo hilo linaloweza kuegeshwa magari 1600 yaliharibiwa.
Wamewataka watu kubaki nyumbani na kufunga madirisha ikiwa wataona moshi kutoka kwa moto huo.

jiunge na group la whatsapp  kupata habari haraka bofya hapa

https://chat.whatsapp.com/4kY5fx3UtyA3xYw5uk3NvF

KWA HABARI ZAIDI

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply