sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » ALIYEMUANDIKIA BARUA OBAMA ATINGA BUNGENI

UNGANA NA 
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA

MWANAFUNZI wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Mlowa wilayani Iringa, Eva Tolage (16) ambaye mwaka jana alimwandika barua Rais Barack Obama wa Marekani akielezea kero zinazowakabili watoto wa kike katika kijiji chake, juzi alitembelea bungeni mjini hapa, huku akiwasisitiza viongozi wa kisiasa kuwajibika kwa kutekeleza ahadi zao ili kuondoa kero zinazowakabili wananchi.

Eva aliyepata pia fursa ya kukutana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na viongozi mbalimbali alisema jambo hilo hakulitarajia, kwani wakati anaandika barua hiyo hakufahamu kuwa itamfikia Rais Obama na kujibu.

Alisema viongozi wa kisiasa wana wajibu mkubwa wa kusimamia ahadi zao ili kuondoa kero vijijini hasa upatikanaji wa maji. Akizungumza wakati wa mahojiano na waandishi wa habari, alisema kero ya maji ni kubwa kijijini kwao ambapo watu na mifugo wamekuwa wakichangia maji.

“Maji ni adimu shuleni, yanapopatikana hadi kijijini kwetu ni kilometa saba hali inayofanya wasichana waishi katika mazingira hatarishi zaidi. Unaweza kupata vishawishi vya wavulana njiani na ukajikuta umepata ujauzito na kushindwa kuendelea na shule.

“Niliamua kumuandikia barua Rais Obama ili atusaidie kupata maji, nilipoandika barua hiyo nikawapatia Shirika la Health Development, lakini nilipopata taarifa kuwa barua hiyo imemfikia Rais Obama nilisikia furaha kwani ni jambo la ajabu sikulitegemea,” alisema.

Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
 +255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call

Karibuni sana
LINK CLASSIC

LIKE PAGE ZETU 



"KWA HABARI ZAIDI "

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply