sponsor

Slider

EMBROIDERY, DTF, & SCREEN PRINTING - T-shirt, Overall, Shirt , Pylon, Kofia Nk..


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » ZIJUE SABABU ZA MIMBA KUHARIBIKA SOMA ZIKO HAPA


Ungana na LINK CLASSIC katika kipengele cha 

ELIMU YA AFYA ZETU
                                                               
topic ni 
ZIJUE SABABU ZA MIMBA KUHARIBIKA SOMA ZIKO HAPA
Kuharibika kwa mimba ni  hali ya mwanamke kupata ujauzito na 
ukatoka kabla ya muda wake ambapo tatizo hili huangaliwa kabla 
ya kutimiza wiki 20 tangu kutungwa kwake.Hali hiyo inapotokea 
huitwa kuwa mimba imetoka au imeharibika (Miscarriage).
Hali hii ya mimba kuharibika inakuwa tofauti kabisa na utoaji 
mimba ambapo kitendo cha kutoa mimba kinafanywa na binadamu 
kwa makusudi na huwa amedhamiria kufanya hivyo.
Akielezea tatizo la mimba kuharibika Daktari Msaidizi w
a Kituo cha Afya Nkwenda Wilayani Karagwe, Dk Aristides 
Ruhikula anasema kuwa katika hali hiyo mtoto anakuwa  hawezi 
kujitegemea mwenyewe kwa mahitaji yanayotakiwa ikiwa ni 
pamoja na kupumua, hivyo hali hiyo ya kutojitegemea husababisha 
kifo.

Sababu za mimba kutoka
Anasema kuwa miongoni mwa sababu zinazosababisha mimba 
kutoka ni pamoja na umri mkubwa ambapo kwa kawaida 
mwanamke anapofikisha umri wa miaka 35 au zaidi 
misuli(sphencters) ya mji wa uzazi hulegea na kupunguza nguvu za
 kuweza kuhimili na kutunza kiumbe kinachokuwa ndani ya mji 
wa uzazi, hivyo kusababisha mimba kutoka.
Hitilafu katika kizazi ambayo huwa katika mfuko wa 
mimba(uterus) ambao muundo wake siyo wa kawaida.Wanawake 
wenye tatizo kama hili huwa na hatari kubwa ya mimba kuharibika 
kabla ya miezi tisa.
Aidha maambukizi ya fangasi au bakteria husababisha misuli ya 
kizazi kushambuliwa hivyo kupoteza uwezo wake wa kuhifadhi 
ujauzito hivyo mimba kuharibika. Miongoni mwa sababu 
zinazosababisha mimba kuharibika ni matatizo ya vinasaba(genetic 
factors)
Hali hiyo hutokana na hitilafu katika kromosomu(cromosomal 
abnormalities) ambayo husababisha vinasaba kuwa katika hali isiyo
 ya kawaida ambayo hali hiyo ni miongoni mwa sababu kubwa 
zinazosababisha mimba kutoka kabla ya kutimiza wiki 13.
Hii husababisha damu ya mama kushindwa kuendana na damu ya 
mtoto hivyo kutokea kwa madhara ambayo humdhuru mtoto na 
kumfanya ashindwe kuhimili hali ya tumboni kwa mama hivyo 
kutoka nje.
Pia ukosefu wa homoni ya progesterone ambayo hufanya kazi 
kubwa tangu kutungwa kwa mimba hadi mtoto kuzaliwa  ambayo 
huchochea uimara wa ukuta wa placenta ambao mtoto hujishikiza.
Upungufu wa homoni hii husababisha ukuta wa mji wa mimba 
kushindwa kuhimili uzito wa mtoto, hali ambayo husababisha 
ujauzito kuharibika kabla ya muda wake.
Sababu nyingine ni utumiaji wa pombe kali, sigara na dawa za 
kulevya. Utumiaji wa vitu hivi huchangia mimba kutoka kutokana 
na kemikali nyingi zilizomo. Hivyo mwanamke mjamzito 
hushauriwa kutotumia  vitu vyenye kemikali, ili kulinda afya yake 
na mtoto aliyeko tumboni.
Pia baadhi ya vyakula na vipodozi huwa vina kemikali ambazo 
hupelekea shingo ya kizazi kulegea na kadiri mimba inavyozidi 
kukua huendelea kuachia na kusababisha mimba kushuka,hali 
inayosababisha mimba kuharibika.

Dalili za mimba kuharibika(symptoms of a miscarriage)
Dk Ruhikula anaeleza kuwa dalili zinazojitokeza  wakati wa 
mimba kuharibika ni pamoja na kutokwa na damu sehemu za siri. 
Hiyo ni dalili kubwa ya mimba kuharibika ambapo damu hiyo 
hutoka sawa na  mwanamke anayekuwa kwenye siku zake.
Maumivu katika viungo ambayo huwa makali katika kiuno, nyonga
 na tumbo chini ya kitovu ambapo maumivu hayo huanza taratibu, 
lakini huongezeka kadiri muda unavyozidi kusonga mbele ambapo 
hali hiyo huambatana na kutokwa damu sehemu za siri.
Dalili nyingine ni kutokwa na uchafu sehemu za siri. Hii ni dalili 
kubwa ya mimba kutoka. Mama mjamzito kuanza kutokwa na 
uchafu mwingi wenye rangi sambamba na mabonge ya damu.
Kupata maumivu ya kiuno huku ukisikia maumivu hayo yanashuka
 chini kwa nguvu fahamu fika mimba yako inaweza kutoka muda 
wowote.

Madhara yatokanayo na kuharibika kwa mimba
Iwapo mama mjamzito amepata tatizo hili  na hajapata tiba sahihi kama kuna mabaki tumboni yanaweza kusababisha madhara mengine ikiwemo kizazi kuoza au kusababisha matatizo mengine kwenye mji wa mimba.
Miongoni mwa madhara yanayoweza kumpata mama ambaye mimba imeharibika ni pamoja na kizazi kuharibika ikiwa mama hatasafishwa vizuri tumboni baada ya mimba kuharibika.
Madhara mengine ni kuugua mfululizo baada ya ujauzito kuharibika pamoja na kushambuliwa na madhara mfululizo baada ya ujauzito kuharibika.
Pia mama anaweza kupata madhara ya kisaikolojia ambayo yanachukua muda mrefu kusahaulika hasa pale wanapokutana na wanawake wajawazito au wenye watoto.

Matibabu 
Mwanamke mwenye tatizo la kuharibika kwa mimba  anaweza 
kupata matibabu kwa njia mbalimbali kutegemea na mgonjwa 
husika.
Matibabu hayo hupatikana hospitalini ambapo mwanamke 
anatakiwa kuwahi pale anapoona dalili hatarishi.
Kwa yule mwenye historia ya kuharibika kwa mimba na tayari ana 
mimba atapata matibabu tofauti na yule mwenye tatizo hilo, lakini hana mimba kwa muda huo.

Ushauri
Dk anasema kuwa dalili zilizotajwa hapo juu peke yake hazitoshi
kuonyesha kuwa mimba imeharibika bali mama mjamzito 
anapoona dalili moja kati ya hizi au zote hata hali ambayo haielewi 
anatakiwa kuwahi hospitalini ili kuweza kupata vipimo.
Endapo mama huyo atachelewa atakuwa anajiweka katika hali 
mbaya kutokana na sumu inayotokana na kiumbe kilichoharibika  
na kusababisha matatizo kwenye mfuko wa uzazi ikiwemo 
ugumba.
Mwanamke yeyote ambaye hajapata tatizo hilo anashauriwa kula 
vyakula kama maboga,  mboga za majani na vyakula vyote 
vinavyojenga mwili.Pia wanatakiwa kuacha matumizi ya vipodozi 
vyenye kemikali  pamoja na uvutaji wa sigara  na dawa za kulevya 
ili kujikinga na tatizo la kuharibika kwa mimba

LINK CLASSIC: Asante sana kwa kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea website hii
Pia waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini





TWITTER    

LINKEDIN     DRIBBBLE

Karibu sana
LINK CLASSIC

BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply