
Ungana
na LINK CLASSIC katika kipengele
cha
HOT NEWZ
topic ni
Ungana na LINK CLASSIC katika kipengele cha
HAKUNA MGAO WA UMEME – TANESCO
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeibuka na kukanusha taarifa zinazoenezwa na baadhi ya wananchi juu ya kuwepo kwa mgao wa umeme kutokana na kukatika kwa umeme kunakoendelea hivi sasa.
Katika mahojiano maalum na mtembezi.com Kaimu Afisa Mahusiano wa Tanesco, Leila Muhaji, amesema kukatika kwa umeme kunasababishwa na uboreshaji wa miundombinu chakavu iliyodumu kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20 na ujenzi wa vituo vipya vya umeme vitakavyofanyakazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha amewataka wananchi kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki cha maboresho yanayoendelea kufanyika na kuahidi mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo watapata umeme wa uhakika na usiokatika mara kwa mara.
Ametoa wito kwa wananchi kushirikiana kwa karibu na shirika hilo hasa katika kipindi hiki cha mvua ili kuweza kutatua kwa haraka changamoto zinazojitokeza katika maeneo mbalimbali.
LINK CLASSIC: Asante sana kwa
kutembelea Website hii coz ni moja ya Support kwetu mungu akubariki sana pia
endelea kusoma na kufungua LEBAL zingine kwani kuna vingi vizuri zaidi ndani ya
Website hii bila kusahau kuwashirikisha ndugu jamaa na marafiki zako kutembelea
website hii
Pia
waweza kuwasilina nasi au kutufollow hapa chini
+255
(0) 652989873 whatsapp
Karibu sana
LINK CLASSIC
BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI
CODE HAPA
No comments: