sponsor

Slider

T - SHIRT PRINTING


LARGER FORMATING

STICKERS BRANDING | LARGE FORMATING


MIFUKO PRINTING

SMALL FORMATING

WEDDING | KITCHEN PART | SEND OFF | INVITATION CARDS

POSTERS | CARTOON | PHOTO PRINTING

» » » DK.KIKWETE ATETA NA WAJUMBE WA NEC,AWAAMBIA “CCM HAITANG’OKA MADARAKANI NG’O”

DSC_2947

UNGANA NA
LINK CLASSIC
KILA SIKU KWA HABARI MPYA

Rais mstaafu wa awamu ya nne  Dk. Jakaya Kikwete  ambaye kesho anatarajia kumkabidhi Rais Dk John Magufuli  nafasi ya juu kabisa ya Uenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, mapema leo Julai 22.2016 katika Makao Makuu ya Chama, Dodoma, wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) amesema kuwa chama hicho kitaendelea kutawala Nchi kutokana na misingi yake imara iliyojiwekea.
Dk. Kikwete ameitoa kauli hiyo wakati wa mazungumzo ya awali muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa NEC mbele ya waandishi wa Habari ambapo ameeleza kuwa, licha ya kuwa na maneno mbalimbali ya mitaani juu ya kukabidhi nafasi hiyo ya Uenyekiti kwa Rais Magufuli, aliwataka wana-CCM kuyapuuza maneno hayo kwani ni ya uongo na wala wasijisumbue nayo.
“Kuna watu wana mitambo yao ya vichochoroni ya kuzalisha bidhaa za uongo uongo tu. Tusiwape nafasi CCM imara na itaendelea kuwa imara Zaidi.
KUna watu walisema CCM itamfia, CCM itakufa,  Kama haikufa sasa basi tena ndio haing’oki ng’o” alieleza Dk. Kikwete.
Katika Mkutano huo, ni wajumbe pekee wa NEC ndio wenye dhamana ya mkutano huo huku tukio kamili la kihistoria la makabidhiano ya kijiti cha Uenyekiti likitarajiwa kufanyika hapo kesho siku ya Jumamosi Julai 23.2016.
DSC_2938
Waziri Mkuu Kasim Majaliwa akisalimiana na wajumbe wa NEC wakati akiwasili kwenye ukumbi wa Mkutano huo.
DSC_2943
Baadhi ya sehemu ya Wajumbe wa NEC
DSC_2931
Mbunge wa Nzega Vijijini na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  na Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na baadhi ya wajumbe wenzake wa NEC
DSC_2940
Meza kuu ikiwasili ukumbini
DSC_2947
Rais mstaafu wa awamu ya nne  Dk. Jakaya Kikwete (katikati) akiongoza kikao hicho cha NEC. Wa kwanza kushoto ni Rais Magufuli, akifuatiwa na Dk. Shein. Na upande wa kulia ni  Katibu Mkuu wa Chama hicho, Mzee Kinana akifuatiwa na Mzee Mangula. (Picha zote na Andrew Chale, Dodoma.
Asante sana kwa kutembelea Website hii Mungu akubariki sana
+255 (0) 652989873 – Whatsapp / Call

Karibuni sana
LINK CLASSIC

LIKE PAGE ZETU 



"KWA HABARI ZAIDI "


BOFYA HAPA KU DOWNLOAD APPS YA LINK CLASSIC USOME HABARI KIRAHISI NA HARAKA ZAIDI

CODE HAPA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply